Tuesday, June 12, 2012

MISS LAKE ZONE INTERCOLLEGES 2012 KUFANYIKA JUNE 23




Kinyang'ayiro cha kumsaka miss lake zone intercolleges 2012 kinatarajiwa kufanyika june 23 mwaka huu mjini Bukoba katika katika ukumbi wa linaz club. Katika shindano hilo ambalo litashereheshwa na mchekeshaji maarufu kama mpoki (Bepari la kihaya), na kuburudishwa na mwanamama malkia wa taarabu nchini ambaye pia ni mshindi wa tuzo za KTMA 2012 Khadija Kopa litawashilikisha warembo kutoka vyuo vilivyopo kanda ya ziwa. Warembo 15 watachuana kugombea umalkia wa vyuo kanda ya ziwa, vyuo vitavyotoa warembo katika shindano hilo ni  CBE, SAUT, Tumaini n Utalii kutoka Mwanza, Open university na SAUT kutoka Kagera na pia watashiriki warembo kutoka Shinyanga. Shindano hilo limedhaminiwa na TBL Kupiti kinywaji chake cha REDDS, Bukoba wadau blogspot, Kasibante FM, Bukoba cable TV, Smart hotel na Kiloyera tours.